Wapo waliosema "SI HASA" kwa makusudi kabisa wakiwa na maana ya kuhusisha neno SIASA. Na hata kwa kizungu wapo waliyosema "POLITRICKS" kwa mtazamo huo huo wakiwa na maana ya "POLITICS".
Katika uwanja wa Siasa huwa panakuwa na mchanganyiko mkubwa sana wa watu wa jinsia mbali mbali, taaluma mbali mbali, vyama tofauti, mikakati tofauti na mambo mengine kadha wa kadha. Cha ajabu ni kwamba wote wanakuwa na mwimbo mmoja "Tunatetea maslahi ya wananchi na kuwaletea mandeleo hao wananchi" Huu wimbo utaimbwa na wote na kila mmoja najitahidi hiyo "Single" ama "Album" yake iwe ndiye imeshika soko.
Mbinu wanazotumia ili kukidhi hayo ambayo ndiyo haki yetu akina yakhe na ndiyo maendeleo yetu, ni kukufanya sisi tuhamasike na maneno ("ambayo mara nyingi hayana vitendo") matamu ama yaliyorembwa na kila ulibwende ambao kwa kipindi kile cha "tabia ya Kinyonga" kuwa na rangi sawa na mahala alipo ili aweze kuwa ama ni mmoja wetu kwa kheri yetu sote ama kwa manufaa yake.
Maana kujibadili kwa rangi kwa kinyonga kuna maana mbili moja kwa faida yake ili apate chakula kwa urahisi anapokuwa katika "Camouflage" ama ajikinge na maadui kwa kutoonekana akiwa katika hiyo camouflage ya jumla pale alipo.!!
Sasa tabia ya wanasiasa haipishani sana na tafsiri ya kinyonga hapo juu. Huu ni wakati sasa tunatakiwa kujua ni wakati gani Kinyonga yu nasi kwa manufaa ya wote na wakati gani yu nasi kwa kujihami yeye binafsi.
Tumeanza kuwachambua mmoja mmoja, lakini si kazi rahisi hata kidogo maana inaonyesha kuwa nao vile vile wamegutuka na wanakuwa "Waangalifu" na si "Waadilifu". Wamekuwa katika makundi ambayo silaha yake ya kujikinga ni "PESA". Wana uwezo wa kuabadili haki kuwa kosa na kosa kuwa haki (hatari kubwa!!).
Pamoja na mapungufu yote ya akina Fidel Castro, Saadam Hussein n.k. lakini bado mimi ningewatumia kufundisha watu vinyonga kama ambao tunao sasa katika nchi yetu.
Nina hakika watu kama hawa "wabunge vinyonga binafsi" tusingekuwa nao na wala wasingepata fursa ya kubwabwaja kama waliyonayo hivi sasa na kutufanya kana kwamba sisi wengine hatujui kutofautisha kati ya zuri na baya ama neno la busara na la kejeli.
Waache waendelee na midomo wazi yao na tamaa zao ila wafahamu kwa sasa hivi Wananchi wa Tanzania si wale wa "ndiyo mkuu" sasa watakuhoji kabla ya yote na watataka kujua kulikoni!!!!!